1Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
3Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
4“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”
5Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
6Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Licensed under CC BY-SA 4.0 (creativecommons.org/licenses/by-sa/4.0).