1Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10
Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Licensed under CC BY-SA 4.0 (creativecommons.org/licenses/by-sa/4.0).
11Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.